Sunday, April 28, 2013

Kikosi cha wana TamTam wakipiga wakipiga dua kwa mungu wao
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Nyota wa watengeneza sukari wa mashamba ya miwa Manungu Turiani mkoani Morogoro, klabu ya Mtibwa Sugar, Hussein Javu amerejea kikosini na kuendelea na mazoezi ya kocha mkuu wa timu hiyo, nahodha wa heshima wa taifa stars, Merck Mexme kwa ajili ya mtanange wa ligi kuu soka Tanzania bara mei mosi mwaka huu dhidi ya vibonde Africa Lyon dimba la Manungu Complex.
Javu ambaye timu nyingi zinamkodolea jicho la tatu ili kuinasa saini yake msimu ujao,  alikuwa anasumbuliwa na majeruhi ya hapa na pale lakini sasa yuko shwari na anapiga jalamba kama kawaida maeneo ya Manungu Turiani.
Akizungumza kwa njia ya simu na MICHEZO BOMBA!  kutoka Manungu, Meneja wa wana TamTam hao, David Bugoya alisema kwa sasa kikosi kipo salama na kinaendelea na mazoezi huku habari njema kwa mashabiki wa klabu hiyo ni urejeo wa mshambuliaji Nguli Hussein Javu.
“Tunamshukuru Mungu tunaendelea vizuri na mazoezi yetu hapa Manungu, vijana wana morali kubwa ambayo inachagizwa na ushindi wa 1-0 mechi iliyopita  dhidi ya Oljoro, pia Javu yupo fiti kuwakabili Lyon mei mosi hapa Manungu”. Alisema Bugoya.
Javu ni miongoni wa washambuliaji walioitwa na Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania “Taifa stars” Mdenish Kim Paulsen ili kuunda kikosi cha Young Taifa stars ambacho kimejumuisha wachezaji vijana na wakubwa ambao hawajapata nafasi ya kucheza timu ya kwanza.
Bugoya aliongeza kuwa mipango yao ni kupata ushindi mnono nyumbani kutokana na mazoezi ya uhakika wanayoyafanya Manungu, lakini alisisitiza kuwa soka lina matokeo ya aina yake hivyo ikiwa tofauti na mipango yao itabidi wakubali hali hiyo.
Afrca Lyon wakiwa chini ya kocha wake Mkenya Charles Otieno jahazi lao linakwenda mrama msimu huu na kuna uwezekano mkubwa wa kushuka daraja kutokana na kuburuza mkia mpaka sasa wakijikusanyia pointi 19 tu.
Mtibwa wapo nafasi ya tano wakijikusanyia pointi 36 na kama watashinda mchezo huo watazidi kujijengea nafasi nzuri ya kusaka nafasi tatu za juu ambapo mapambano ni baina ya klabu za Coastal Union “wagosi wa kaya”, Wana “Nkulukumbi” Kagera Sugar, Simba na Azam Fc “wana lambalamba”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video