Friday, April 26, 2013

azam fc vs coastal mapinduzi cup 2013
Na Baraka Mpenja
Wakati Watanzania wakiadhimisha miaka 49 ya Muungano, kwa wale wapenda kandanda watakuwa wanafuatilia mechi ya kukata na shoka baina ya Wagosi wa Kaya wanaonolewa na kocha Hemed Morroco dhidi ya wana lambalamba kutoka Chamazi Klabu ya Azam fc dimba la Chama cha Mapinduzi Mkwakwani jijini Tanga “Waja leo waondoka” leo.
Mchezo wa leo ni mgumu sana kwa timu zote kutokana na uhitaji mkubwa wa mzigo wa pointi tatu kwa timu zote ili kujiweka mazingira mazuri katika msimamo wa ligi ambapo Azam wanawania ubingwa na Coastal wanahitaji nafasi ya pili.
Endapo  wana lambalamba watashinda leo watafikisha poinbti 50 nyuma ya Yanga wenye pointi 56 kileleni na wakihitaji pointi moja tu katika michezo miwili iliyosalia ili kujitangazia ubingwa msimu huu wa 2012/2013.
Kila kukicha Azam wanamwombea dua mbaya Yanga ili apoteze michezo miwili ijayo dhidi ya Coastal Unioni na Mnyama Simba hivyo kuwa na matumaini ya kupata ubingwa wao wa kwanza tangu waanze kushiriki michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2007/2008.
Wawakilishi hao pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa wanapigana kufa na kupona ili kuweka historia ya kutwaa ndoo yaligi kuu ambayo mabingwa watetezi  Simba wapo chali na wamekubali kuupoteza.
Wakati huo huo Viongozi saba wa klabu ya Azam fc wakiongozwa na katibu mkuu wa klabu hiyo Alhaji Idrisa Nassor wanakwenda nchini Morroco leo kwa lengo la kufanya maandalizi ya mwanzo kabla ya timu yao kusafiri jumanne ya wiki ijayo.
Afisa habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga alisema wanaondoa leo kwa ndege ya Emirates saa 11 jioni uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere Dar es salaam.
“Hata viongozi wa serikali wanaposafiri kwenda sehemu Fulani kufanya ziara wanatuma watu kwa sababu za usalama, sisi pia kwa kufuata utamaduni huo lazima baadhi yetu tuwahi kule kuangalia nini kinachoendelea huko ”. Alisema Idd.
Idd aliongeza kuwa kila wanapoenda ugenini lazima watangulize viongozi  na baadaye timu inapokelewa nao.
Afisa habari huyo aliwataka watanzania kuwaombea dua njema kwani hawatawaangusha hata kidogo kutokana na uwezo wa timu yao na maandalizi kwa ujumla.
“Walikuja hapa AS FAR Rabat tukatoa nao suluhu, siyo mbaya sana kwetu, tunahitaji ushindi wowote , kama tutapata bao moja la ugenini, tutawachanganya zaidi wapinzani wetu, tuombeane watanzania wote”. Alisema Idd.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video