Monday, April 29, 2013

6
ABDALLAH KIBADENI “KING MPUTA” (MWENYE KOFIA)
TFF Kagera Sugar 
Kikosi cha Kagera Sugar katika moja ya mechi za nyuma za ligi kuu Tanzania bara

Na Baraka Mpenja
Watengeneza sukari wa kaitaba mkoani Kagera, klabu ya Kagera Sugar tayari imeshawasili mkoani Morogoro kujiandaa na mchezo wao wa jumatano ya wiki hii uwanja wa Jamhuri dhidi ya maafande wa Polisi Morogoro ambao jana wametandikwa bao 2-1 na Mnyama Simba na kuzidi kupoteza matumaini ya kusalia ligi kuu bara msimu huu.
Akizungumza na MICHEZO BOMBA! kocha mkuu wa wana “Nkulukumbi” Kagera Sugar Abdallah King Kibadeni “Mputa” alisema timu imewasili usiku wa jana na leo wanatarajia kufanya mazoezi katika uwanja wa Jamhuri.
“Timu iko salama, tunajiandaa kupambana na Polisi Morogoro ambao wanahitaji ushindi kwa vyoyote vile hususani baada ya kufungwa jana na Simba, tunatambua watapigana kufa na kupona lakini tuko shwari”. Alisema Kibadeni Kutokea mkoani Morogoro.
Kibadeni mwenye ndoto za kushika nafasi ya pili msimu huu alisema kuwa kabla ya kusafiri kwenda Mji kasoro bahari walipitia mkoani Gieta ambapo walicheza mechi mbili za kirafiki ili kupima ubavu kikosi chao.
“Tumetokea Gieta, tumecheza mechi mbili, moja ilikuwa dhidi ya kikosi cha vijana chini ya miaka 20 wa mkoani Geita na tukawafunga mabao 2-0 na ya pili tulicheza na wachimba madini wa Mgusi FC na kuwafunga mabao 2-1, mechi hizi zimenisaidia kutambua makosa ya wachezaji wangu”. Alisema Kibadeni.
Kagera sugar inajiandaa kupambana na Polisi Moro ambayo ipo nafasi ya pili kutoka mkiani akijikusanyia pointi 19 baada ya kutandikwa na simba mabao2-1 katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam jana.
Kwa mujibu wa Viongozi wa Polisi Moro, tayari wameshakiri kuwa wana uwezekano mkubwa wa kutoa mkono wa bai bai kwa michuano ya ligi kuu Tanzania bara msimu huu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video