Monday, April 22, 2013

>>BADO YUPO UCHUNGUZI FIFA TUKIO LAKE KUPIGA NGUMI URUGUAY v CHILE!!
>> GRAEME SOUNESS ASEMA HASTAHILI KUCHEZA ANFIELD!!
>>PATA VIMBWANGA 10 VYA SUAREZ!!
EVRA_N_SUAREZWAKATI Meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers, akikiri kutoona tukio la Straika wake Luis Suarez kuonekana akimng’ata Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic bila Refa Kevin Friend kuona, FA imesema itapitia Mkanda huo na Ripoti ya Refa ili kutoa mwelekeo huku Wachambuzi wa Soka huko England wakilaani vikali kitendo hicho.
Brendan Rodgers ameahidi kupitia Mkanda wa Video wa tukio hilo na kutoa tamko lakini Meneja wa zamani wa Liverpool, Graeme Souness, amelaani vikali tukio hilo na kusema umefika wakati wa Mchezaji huyo kutoka Uruguay kuondolewa Liverpool.
Souness ameng’ang’ania kuwa Liverpool ni Klabu kubwa yenye hadhi kama Barcelona, Real Madrid a Manchester United, na Mchezaji huyo anatia dosari sifa ya Klabu.
Tukio hilo la Suarez kumng’ata Ivanovic lilitokea kwenye Mechi ya BPL, Barclays Premier League, iliochezwa Anfield na Liverpool kutoka sare 2-2 na Chelsea huku Suarez akishika makusudi na Chelsea kupata Penati waliyofunga na ni yeye Suarez ndie alieisawazishia Liverpool katika Dakika za majeruhi.
PATA MATUKIO YA UTATA YA SUAREZ KATIKA ULIMWENGU WA SOKA:
Novemba 2007
Akiwa Nahodha wa Ajax alifungiwa na Klabu yake baada ya kupigana na mwenzake Albert Luque wakati wa Haftaimu kwenye Mechi.
Julai 2010
Afrika na Dunia nzima itamkumbuka Suarez, ambae ni Mchezaji wa Uruguay, kwa kuikatili Ghana huko Afrika Kusini kwenye mechi ya Robo Fainali ya Kombe la Dunia alipoushika mpira kwa makusudi kwenye mstari wa goli dakika ya mwisho ya muda wa nyongeza na kuwanyima Ghana goli la wazi la ushindi.
Kwa kitendo hicho, Suarez aliwashwa Kadi Nyekundu na Ghana kupewa penati lakini Asamoah Gyan, ambae aliwahi kuwa Ligi Kuu England na Timu ya Sunderland, alikosa kufunga penati hiyo.
Novemba 2010
Alipata Kifungo cha Mechi 7 akiwa huko Uholanzi  na Klabu ya Ajax baada ya kumng’ata meno Mchezaji wa PSV Eindhoven Otman Bakkal kwenye mechi ya Ligi huko Uholanzi.
Octoba 2011
Wakicheza na Everton, alivunga amechezewa faulo na Jack Rodwell na kujidondosha na Rodwell akapewa Kadi Nyekundu.
Octoba 2011
Suárez alimkashifu Kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United na kufungiwa Mechi 7 na kupigwa Faini Pauni 40,000.
Decemba 2011
Akiwa kwenye mashitaka ya kumkashifu Kibaguzi Patrice Evra wa Manchester United na kabla hajahukumiwa alionekana kutoa ishara ya matusi kwa Mashabiki wa Fulham kitendo ambacho kilimpa Kifungo cha Mechi 1.
Februari 2012
Man United na Liverpool walikutana tena Old Trafford kwa mara ya kwanza tangu tukio la Suarez kumkashifu Kibaguzi Evra na Suarez, bila kutarajiwa, aligoma kumpa mkono Evra.
October 2012
Alishangilia Goli lake kwa kujirusha mbele ya Meneja wa Everton, David Moyes, ambae kabla ya Mechi hiyo na Liverpool alitamka Wachezaji wadanganyifu kama Suarez wnaohadaa Marefa wanafanya Mashabiki waikatae Soka ya England.
Januari 2013
Alipoza mpira kwa mkono na kufunga Bao la ushindi kwa Liverpool kwenye Mechi ya Raundi ya 3 ya FA CUP dhidi ya Timu ya Daraja la chini Mansfield.
Machi 2013
Akiichezea Nchi yake Uruguay kwenye Mechi ya Mchujo ya kuwania kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014, Suarez alionekana kumtandika ngumi Beki wa Chile Gonzalo Jara bila Refa kuona.
FIFA wanachunguza tukio hili.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video