Soka kimataifa na Francis Kivuyo.

Baada ya FC Barcelona maarufu kama Wakatalunya kutoka vichwa chini mikono nyuma dimbani Allianz Arena jana baada ya kuchezea kichapo cha mbwa koko cha magoli 4-0 kutoka kwa Bayern Munich kwenye michuano ya kuwania hatua ya faili ya klabu bingwa barani Ulaya, sasa ni zamu ya Real Madrid na Borussia Dortmund kukipiga kesho.
Goli la kwanza la Bayern Munich lilipatikana kupitia; T.Muller mnamo dakika ya 25 ya mtanange, la pili likatupiwa kambani na Gomez dakika ya 49,Arjen Robben pia akatupi la tatu dakikaya 73 huku la nne na la mwisho likivurumishwa kimyani kwa mara nyingine tena na T.Muller
Mchezo ulikuwa mgumu kwa pande zote mbili, huku Barcelona kama kawaida yake akioneka kumiliki mchezo sana katika kipindi cha kwanza lakini akijikuta anapigwa goli la kwanza mapema dakika ya 25 ya mchezokupitia mshambuliaji hatari T.Muller.
Sasa wakati FC Barcelona ikisikilizia maumivu makali, wanatarajia kuwapokea Bayern Munich kwenye mtanange wa kurudiana utakaopigwa dimbani Nou Camp siku chache baadaye.
HIVYO NDIVYO MAMBO YALIVYOKUWA HUKO ARENA NCHI UJERUMANI
![]() | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Wachezaji wa Bayern wakianza kushanglia goli la kwanza lilifongwa na Thomas Muller. |
SHUGHULI ILIKUWA NZITO KWA UPANDE WA FC BARCELONA
![]() |
Lionel Messi. |
0 comments:
Post a Comment