Saturday, April 20, 2013


John-Boko-Azam-fc1
Na Baraka Mpenja
Leo hapatoshi uwanja wa taifa majira ya saa kumi kamili jioni ambapo wawakilishi pekee wa Tanzania michuano ya kimataifa barani Afrika, klabu ya Azam FC itakuwa na kibarua kizito mbele ya timu ya jeshi la Morroco, AS FAR Rabat, katika dimba la taifa jijini Dar es salaam.
 Azam FC ina fursa nzuri ya kufanya vizuri kwenye mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Emile Fred kutoka Shelisheli kutokana na maandalizi iliyofanya.
 Makocha wasaidizi wa timu zote mbili, Kalimangonga Ongala wa Azam na Lahcen Ouadani wa AS FAR Rabat walizungumza jana na waandishi wa habari kuhusu mechi hiyo, kuwa wamejiandaa kuibuka na ushindi.
Kocha Ongala alisema wamepata DVD za mechi tatu za mwisho za AS FAR Rabat, moja ikiwa dhidi ya timu ya Al Nasir ya Libya ambayo waliitoa katika raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho na nyingine mbili za ligi ya Morocco ambazo wanazifanyia kazi kuhakikisha wanashinda kesho.
Naye Ouadani alisema hawaifahamu vizuri Azam, lakini wanaujua mpira wa Tanzania baada ya kuangalia mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Morocco (Lions of the Atlas) iliyochezwa jijini Dar es Salaam Machi 24 mwaka huu na Stars kushinda mabao 3-1.
 Baadhi ya wachezaji ambao Azam inatarajia kuwatumia kwenye mechi ya leo ni pamoja na Aishi Manula, Mwadini Ally, Khamis Mcha, John Bocco na Salum Abubakar ambao pia wamo kwenye kikosi cha sasa cha Taifa Stars kilicho chini ya kocha Kim Poulsen.
 AS FAR Rabat ina wachezaji sita kwenye timu ya Taifa ya Morocco. Wachezaji hao ni mabeki Younes Bellakhdar, Abderrahim Achchakir, Younnes Hammal, na viungo Salaheddine Said, Salaheddine Aqqal na Youssef Kaddioui.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video