Saturday, April 27, 2013

P1230620
Na Baraka Mpenja
Wajelajela Tanzania Prisons kutoka jijini Mbeya “Jiji la kijani” wanatarajia kuanza safari yao hapo kesho kuja jijini Dar es salaam kwa ajili ya mchezo wao wa ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Maafande wa jeshi la kujenga Taifa JKT Ruvu dimba la Chamazi Mbande nje kidogo ya jiji la Dar es salaam siku ya mei mosi mwaka huu.
Katibu mkuu wa Tanzania Prisons Sadick Jumbe  ameiambia MICHEZO BOMBA!  kuwa  kikosi chao mpaka sasa kipo salama na kimejiandaa kwa muda mrefu kuwakabili JKT Ruvu ambao kwa sasa wana morali kubwa ya kupambana kubakia ligi kuu msimu kutokana na kupata matokeo ya ushindi mchezo uliopita dhidi ya vibonde wa Ligi hiyo Africa Lyon ya jijini Dar es salaam.
“Kocha wetu Jumanne Chale amefanya mazoezi ya nguvu kujiandaa na mchezo huo, tuko nafasi ya tisa kati ya timu 14 tukiwa na pointi 26 sawa na wapinzani wetu, lakini malengo yetu ni kushinda mchezo huo ili kujiweka nafasi nzuri katika msimamo wa ligi”. Alisema Jumbe.
Katibu huyo aliongeza kuwa kwa sasa timu ina morali kubwa kutokana na wadau wa jijini Mbeya kujitokeza kwa wingi kuwapa sapoti wakiongozwa na kamanda wa polisi mkoani humo, Diwani Athman Msuya ambaye anaongoza kamati ya saidia Prisons ishinde.
“Tunakuja Dar es salaam tukiwa kamili gado, lazima niwaambie mashabiki kwamba kikosi chetu kwa sasa kipo imara na wachezaji wote wapo katika hali nzuri, tutapambana sana na maafande wenzetu ili kupata matokeo ya ushindi”.
Wakata huo huo maafande wa JKT Ruvu wakiwa chini ya mwalimu Keny Mwaisabula ”mzazi” na msaidizi wake Greyson Haule wanaendelea na mazoezi kujiandaa na matanange huo wa kukata na mundu.
Akizungumza leo hii, Haule ambaye ni kocha msaidizi wa klabu hiyo alisema wana uhakika wa kupata matokeo ya ushindi mbele ya Prisons kwani kikosi kipo sawa ka mechi zote zilizosalia.
“Tuliwafunga Lyon na kupata pointi tatu na kufikisha 26 sawa na Prisons, hakika tunasakama kwa nguvu zote pointi nyingine tatu mbele ya wanajeshi wenzetu, lazima tuwaadabishe siku hiyo”. Alisema Haule.
Timu hizo mbili zote zina pointi 26 katika nafasi ya tisa na kumi, lakini Prisons wapo juu ya Ruvu kufuatia wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video