Monday, April 22, 2013


1
KENY MWAISABULA "MZAZI"
Na Baraka Mpenja
Wakati maafande wa JKT Ruvu kutoka mkoani Pwani wakihaha kujinusru kubakia ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu 2012/2013, kocha wake mpya Keny Mwaisabula “Mzazi” amesema malengo yake makubwa ni msimu ujao kwani kwa sasa hana uwezo wa kubadili kikosi chake.

Akizungumza na MICHEZO BOMBA! leo hii, Mwaisabula ambaye timu yake ilipoteza mchezo wake muhimu jana kwa kufungwa na vinara Yanga mabao 3-0 alisema amekubali majukumu ya kuinoa klabu hiyo na taratibu zote za mkataba wake zimekamilika.

“Kwa sasa ninahusika kutoa ushauri kwa timu yangu kwani ndio kwanza nimeanza kazi, hakika muda huu hautoshi kwangu hivyo najiandaa na msimu ujao wa ligi”. Alisema Mwaisabula.

Kocha huyo ambaye pia ni mjumbe wa kamati inayoratibu sherehe za mei mosi mwaka huu zitakazofanyika kitaifa jijini Mbeya, aliongeza kuwa licha ya timu yake kuwa na pointi 23 katika nafasi ya 11 ya msimamo wa ligi kuu bara, mategemeo yake ni kufanya vizuri mechi zilizosalia ili kujihakikishia nafasi ya kubakia ligi kuu.

“Tunajiandaa na mchezo wa keshokutwa dhidi ya Africa Lyon, tumepoteza jana dhidi ya vinara Yanga, sasa hesabu zetu ni kupata pointi tatu ili kufikisha 26 na kuendelea kujiweka salama, wachezaji wapo salama na wana morali ya kuikoa timu yao”. Alisema Mwaisabula aliyewahi kuifundisha Yanga.

Aidha Kocha huyo aliyewahi kuzifundisha klabu za Africas Lyon, Villa Squad, na nyinginezo aliwataka mashabiki wa soka mkoani Pwani kuondoa hofu kwani watajitahidi kufanya vizuri zaidi ili kuwafurahisha msimu ujao.

Mwaisabula amerithi mikoba ya kocha aliyebwaga manyanga kuwanoa maafande hao wa JKT Ruvu, Mwalimu Charles Kilinda.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video