Tuesday, April 23, 2013

Musa Hassan Mgosi Kulia

Na Baraka Mpenja
Nguli wa kusakata kabumbu na aliyewahi kutamba na klabu ya Simba, DC Mote Mapembe ya Kongo na sasa yupo na JKT Ruvu Musa Hassan Mgosi “Mgunya” amesema kesho ni kesho lazima awapoteze Lyon kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara ndani ya dimba la Chamazi mbande nje kidogo ya jiji la Dar es salaam dhidi ya klabu ya Africa Lyon.
Mgosi ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa anajisikia vibaya sana timu yake kufungwa na Yanga 3-0, na  sasa hesabu zake ni kufuta machungu hayo mbele ya wapinzani wao wakubwa katika mchezo wa kesho.
“Endapo Lyon watatufunga watakaa juu yetu, na sisi tukipata matokeo ya ushindi tutajiweka mahali pazuri, wachezaji wote tunajua wajibu wetu na kesho ni shughuli moja ya kutafuta ushindi tu”. Alisema Mgosi.
Nyota huyo mwenye uchu wa kufunga magoli aliongeza kuwa yeye ni mchezaji mwenye mbinu nyingi za kufumania nyavu na kesho itatumia mbinu zake za Kongo na simba miaka ya nyuma kuwazamisha Lyon.
“Mara nyingi natumia muda wangu kuwaambia wachezaji wenzangu kuwa soka lina matokeo matatu, kufunga, kufungwa na kutoa sare ama suluhu, tukifungwa tunayaacha uwanjani na kwenda kujifua upya, nafikiri wamenielewa na kesho tutacheza kwa ushirikia’.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video