Tuesday, April 30, 2013

IMG_8579
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Mashindano ya vijana chini ya miaka 14 na 20 yanayoratibiwa na chama cha soka la vijana wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam yamesogezwa mbele ambapo sasa yataanza kutimua vumbi mei 4 badala ya mei mosi mwaka huu katika dimba la kumbukumbu ya Hayati Karume.
Mwenyekiti wa chama cha soka la vijana Ilala (IDYOSA) Faza Edwirn Mloka ameiambia MICHEZO BOMBA!  kuwa katika kikao cha kamati yan mashindano kilichofanyika hivi karibuni timu shiriki ziliomba kusogezwa mbele ili kuwaandaa vizuri vijana wao, na wao wamekubaliana nao  na kutoa nafasi hiyo kwao.
“Klabu zimeomba kujiandaa vizuri na sisi tumesogeza siku, hapo kesho mei mosi tunakutana ofisi za TFF karume saa tatu asubuhi kupanga ratiba ambapo makocha na makatibu wa timu watahusika”. Alisema Mloka.
Mloka alisema mwaka huu wanatarajia kuendesha mashindano yenye mvuto zaidi na kufuata kanuni zilizowekwa na chama hicho;
“Hatutaki vijeba katika michuano hii, tumefanya usaili makini sana wa wachezaji, kila atayecheza ana umri sitahiki na hivi ndivyo tunavyotaka, hakuna shaka kila kitu kitaenda shwari”. Alisema Faza Mloka akiwa na uhakika.
Pia mwenyekiti huyo aliwataka wadau na wapenzi wa kandanda kutupia macho yao katika mashindano haya kwani ndio chimbuko la baadhi ya wachezaji wanaofanya vizuri sana ligi kuu soka Tanzania bara.
“Huwezi kumtaja bwana mdogo Salum Abubakar “Sure boy” au Frank Domayo wa Yanga bila kuhusisha michuano ya vijana Ilala, hapa ndio chimbuko la nyota hawa na wengine wengi, ni muhimu kujitokeza kuwasaidia vijana wetu”. Alisisitiza Mloka.
Baada ya michuano hii chama cha soka manispaa ya Ilala kimealikwa mwezi juni mkoani Tabora kushiriki michuano ya vijana ya mkoa huo kama sehemu ya kubadilishana uzoefu wa uongozi wa soka la vijana pamoja na kudumisha umoja na mshikamano.
Soka la vijana kwa sasa ndio msingi wa soka duniani kote na kila taifa sasa linawekeza huko, huku Tanzania pia tukifuata nyayo zao tukiongozwa na Rais wa TFF anayemaliza muda wake Injinia Leodigar Chilla Tenga ambaye hivi karibuni ametoa mipira 1200 iliyogharimu dola elfu tatu ili igawiwe shule za misingi na vituo vya soka mikoa yote ya Tanzania.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video