SERGIO KUN AGUERO |
Kocha msaidizi wa klabu ya Manchester City ya England Brian
Kidd amesema bado kocha mkuu Roberto Mancini anaamini timu yake itatetea
ubingwa ligi kuu nchini England.
Kidd anasema Mancini anajua matokeo yaliyo kinyume na
ushindi dhidi ya Tottenham siku ya jumapili ni sawa na kuwakabidhi ubingwa
mapema vinara Manchester United endapo watashinda dhidi ya Aston
Villa siku ya Jumatatu.
Man City watakuwa wakiangalia maendeleo ya washambuliaji wao
Sergio Kun Aguero na David Silva kujua namna ya kuwatumia wakitokea katika
majeraha.
Tottenham itamkosa mshambuliaji wake tegemeo Jermaine Defoe
ambaye ni majeruhi huku Aaron Lennon akijikongoja kutoka katika hali hiyo pia
Gareth Bale atarejea dimbani kwa mara ya kwanza baada ya kutoka kuwa majeruhi.
Manchester United imecheza mechi 33 ambapo inaongoza ikiwa
na pointi 81 ikifuatiwa na mabingwa watetezi Man City wenye pointi 68 lakini
wamecheza mechi 32.
Mchuano Mkali zaidi
Timu hizo zinachuana vikali kuwania ubingwa unaoshikiliwa
timu hizo hasimu zinazotoka jiji moja la Manchester ambapo ubingwa lazima utue
jijini humo lakini ni timu gani itauchukua ni utakaotoa jibu kwa mechi
zilizosalia.
Katika kinyang’anyiro cha kushiriki ligi ya mabingwa Ulaya
kumebaki nafasi tatu kwa Chelsea,Arsenal,Tottenham Hotspurs na Everton.Timu nne
tu zinatakiwa zitakazoshindwa basi zitalazimika kupigania nafasi ya kushiriki
Europa League maarufu kwa hapa nyumbani kama UEFA NDOGO.
Jermaine Defoe kushoto |
0 comments:
Post a Comment