Tuesday, April 30, 2013

Wachezaji wa klabu ya Yanga ambao ndio mabingwa wa liku kuu soka Tanzania bara msimu wa 2012/2013 wakiweka miili sawa, wa kwanza kulia ni kiungo tegemeo wa klabu hiyo Mnyarwanda Haruna Hakizima Fadhil Niyonzima maarufu kama Fabrigas, naye atakuwepo hapo kesho kupambana na wagosi wa kaya SONY DSC 
Kikosi cha Wagosi wa kaya, Wagosi wa Ndima kutoka jiji la Tanga, hawa ndio walichangia kuwapa ubingwa Yanga wiki hii baada ya kuwabana Azam, sasa wanashuka ugani kesho dhidi ya mabingwa hao

Na Baraka Mpenja
Wakiwa tayari mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2012/2013, wanajangwani Dar Young Africans wamesema mchezo wao wa mei mosi dhidi ya wagosi wa ndima wagosi wa kaya Caostal Union kutoka jijini Tanga “waja leo waondoka leo” ndani ya dimba la kisasa la taifa jijini Dar es salaam utakuwa maalumu kwa mashabiki wa klabu huyo kufurahia pamoja ubingwa wao huku timu yao ikiwa inaendelea kufanya vizuri.
Afisa habari wa mabingwa hao waliotwa taji mara 24 liku kuu, Baraka Kizuguto ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa baada ya kuwapoka ubinwgwa watani zao wa jadi, sasa wanataka kuwafurahisha mashabiki wao katika michezo yao miwili iliyosalia.
Yanga wamebakiza mechi mbili baina ya Wagosi wa Kaya ambao watakwaruzana nao kesho taifa na mchezo wa mwisho utawakutanisha na watani zao wa jadi wekundu wa msimbazi Simba wenye kumbukumbu ya kuwachapa kipigo cha mbwa mwizi cha mabo 5-0 msimu wa mwaka jana.
“Licha ya kuwa mabingwa Yanga hatubweteki hata kidogo, tunaanza kugawa dozi kwa wagosi wa kaya na baada ya hapo tunaanza kuwawinda Simba ambao kuwafunga itaongeza raha ya ubingwa wetu”. Alisema Kizuguto.
Kuhusu hali ya wachezaji, Kizuguto alisema wote wapo salama na wana morali kubwa sana kuwavaa wapinzani wao waliochangia kuwapa ubingwa baada ya kuwabana waliokuwa wapinzani wao wakubwa Azam fc  “Lambalamba” kwa kutoka nao sare ya bao 1-1 dimba la chama cha Mapinduzi (CCM) jijini Tanga.
“Tumefanya mazoezi vizuri, wachezaji kwanza wana furaha ya kutwaa ubingwa, lakini wanaahidi kuwa ili kunogesha utamu wa ubingwa wao lazima washinde kesho na mechi ya Simba”. Alisema Kizuguto kwa kujiamini.
Wakati Yanga wakitamba kuibuka kidedea hapo kesho, kwa upande wa Coastal union wamesema maandalizi yamekamilika kwa asilimia kubwa.
Kocha mkuu wa klabu hiyo Hemed Morroco ameimabia MICHEZO BOMBA! kuwa licha ya waamuzi kuvurunda baadhi ya michezo wao wamejipanga kwa uzuri sana kukabiliana na Yanga hapo kesho uwanja wa taifa.
“Siku tumecheza na Azam nyumbani waamuzi walichemsha sana na kusababisiha tushindwe kupata ushindi, hakika tulistahili kuwafunga, sasa tuna kazi nyingine na Yanga sijui itakuwaje, lakini tumejipanga kwa lolote lile”. Alisema Morroco kwa kujiamini.
Coastal union wamejikusanyia pointi 36 katika nafasi ya tano,  juu yao wapo Simba wenye pointi  39 katika nafasi ya nne huku Kagera Sugar wakiwa nafasi ya tatu na pointi 40  na Azam wapo nafasi ya pili na mzigo wa pointi 48.
Kesho mashine za Yanga kama Haruna Niyonzima “Fabrigas”, Khamis Kiiza, Saimon Msuva, Athman Idd “Chuji”, Frank Domayo, Kelvin Yondan, Canavaro na wengine wengi wataongoza kikosi chao kupepetana na Wagosi wa ndima kutoka Tanga.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video