Monday, April 29, 2013

DSC04831 - Copy
Na Baraka Mpenja
Waburaza mkia wa ligi kuu soka Tanzania bara, klabu ya Africa Lyon ya jijini Dar es salaam sasa wameanza kujiandaa kucheza ligi daraja la kwanza baada ya kupumua kwa mashine dakika hizi za lala salama.
Kocha mkuu wa klabu hiyo Mkenya Charles Otieno ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa timu yao sasa ina aslillimi tano kati ya mia moja kuabkia ligi kuu huku wakiongoza kwa kufungwa mabao mengi zaidi ya timu zote.
Otieno alisema hali yao ni ngumu sana hivyo wanajipanga kwa lolote kwani katika mechi mbili zilizosalia wanaweza kufikisha pointi 25 pamoja na wapinzani wao polisi morogoro,na Toto Africans, lakini Mgambo akipata moja tu hawa ujanja.
“Ukiangalia jinsi ligi inavyokwenda endapo Mgambo atapata pointi moja katika michezo yake iliyosalia, basi sisi, Toto na Polisi ndio hivyo tutaenda kujipanga ligi daraja la kwanza”. Alisema Otieno.
Kocha huyo aliongeza kuwa timu haina matatizo makubwa sana lakini kubwa zaidi ni sehemu ya ushambuliaji ambayo inapata nafasi nyingi na kushindwa kuzitumia.
Otieno alisisitiza kuwa watu wengi wanaona itakuwa vibaya sana kurudi ligi daraja la kwanza, lakini kiukweli hawana jinsi na lazima wajiandae kulingana na msimamo ulivyo.
“Mimi nitabaki na timu mpaka mwisho, tukishuka daraja tutajipanga ndani ya mwaka mmoja na kurudi ligi kuu tena, timu ina hela za kuwalipa wachezaji mishahara, posho, usafiri na mtu akisema tuna matatizo ya pesa sio sahihi”. Alisema Otieno.
Akiongelea saula waamuzi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Otieno alisema waamuzi wengi wanachezesha ovyo na kushindwa kutafsiri kwa ufasaha sheria 17 za kandanda.
Lyon mpaka sasa ipo mkiani ikijikusanyia pointi 19 na dalili zote zimeshawadia, wanaweza kushuka daraja na kupisha timu za Mbeya City, Rhino Rangers na Ashanti United zilizopanda daraja msimu huu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video