Friday, April 5, 2013



Na Baraka Mpenja, Dar es Salaam
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya mchezo wa Tenisi Tanzania, Kiango Kipingu, amewataka wadau wenye nia ya kuendeleza mchezo huo kujitokeza kuomba nafasi za uongozi ndani ya chama cha Tenisi Tanzania ili kuinua kiwango cha mchezo huo unaoonekana kushuka sana.
Kipingu amesema kuwa  imefika wakati wa kupata viongozi ambao sio wachumia matumbo yaani wanaojali zaidi maslahi binafsi na kusahau majukumu yao ya kuendeleza mchezo huo.
“Unajua hali ya Tenisi Tanzania ni mbaya sana, hakuna watu wenye udhati wa kuinua mchezo huu, hivyo ni muhimu watu wakajitokeza kuingia katika mchezo wa tenisi ili kufikia mafanikio makubwa zaidi”. Alisema Kipingu.
Kocha huyo aliyeanza kucheza mchezo huo miaka 20 iliyopita mjini Morogoro na baadaye 1996 shirikisho la mchezo huo duniani ITF kumpeleka Afrika kusini kucheza mchezo huo, alisema banafsi hakupanga kuingia katika kazi ya ukocha, lakini ubabaishaji mkubwa nchini Tanzania ndio siri ya yeye kujimwaga katika ukocha.
“Nchi yetu iko nyuma sana, hakuna ubunifu wa mashindano mbalimbali, vijana wanakatishwa tamaa kwa kukosa milango ya kutokea,  hakika nikaamua kuachana na uchezaji na kuingia katika ukocha”. Aliongeza kipingu.
Kipingu ambaye aliishi kwa muda mrefu nchini Afrika kusini katika mji wa Pretoria na kucheza mchezo huo kwa mafanikio, alisisitiza kuwa lengo lake lilikuwa kushiriki michuano ya Wembleydone, lakini safari imekuwa ndefu na sasa anawaza kulisaidia taifa kuhamasisha mchezo huo.
Akizungumzia mipango yake, Kipingu alisema anahitaji kuanzisha kituo chake cha kuibua na kulea vipaji, ingawa bado ana safari ndefu sana kutokana na kukosekana kwa masaada kutoka kwa wadau na viongozi wa serikali.
Pia alisema kuwa kwa sasa anaendesha programu za mchezo huo katika timu tofauti, shule tofauti za msingi, lakini malipo yake yamekuwa ya kusuasua sana.
Kipingu alisisitiza kuwa yeye ana uwezo mkubwa sana, lakini kinachomwangusha ni hali ya viongozi kutothamini makocha wazawa.
“Angalia timu ya vijana ilivyofanya vizuri hivi karibuni katika mashindano ya kanda ya tano afrika, lakini juzi juzi wameleta kocha wa kigeni kutoka Msiri, amekula fedha nyingi bila kazi ya maana, mimi ambaye nafundisha timu mbalimbali akiwemo ya taifa kwa mafaniko nadharauliwa.”Aliongeza Kipingu.
Kocha huyo mwenye moyo wa kujitolea alisema ni wakati mwafaka kwa viongozi wa mchezo huo kuweka mikakati maalumu ya kuendeleza mchezo huo kwa kushirikiana na watu binafsi wenye nia kama yeye.
Pia alisema yeye alizaliwa Kigamboni jijini Dar es Salaam hivyo anataka kupeleka kituo cha mchezo huo katika kitongoji chake, na aliwataka watu wengine kuiga mafano huo ili kuyafikia maeneo mengi ya Tanzania.

 

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video