Sunday, April 28, 2013

Kocha msaidizi wa Simba Julio (kulia) akiwa na afisa habari wa klabu hiyo, Ezekiel Kamwaga eee
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Mikikimikiki ya ligi kuu Vodacom Tanzania bara inatarajia kuendelea jioni ya leo katika dimba la taifa ambapo waliokuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo, wekundu wa msimbazi Simba “Taifa kubwa” watawakaribisha wapiga kwata wa Polisi Morogoro katika dimba la taifa maeneo ya Chang`ombe jijini Dar es salaam.
Mchezo huo unatarajia kuwa mkali kutokana na umuhimu wa matokeo ya ushindi kwa timu nzote mbili.
Mnyama Simba ambaye tayari ameshapoteza ubingwa wake na kuwakabidhi watani zake wa jadi Dar Young Africans “Kwalalumpa Malysia” anahitaji ushindi kufa na kupona ili kupigania angalau nafasi ya pili na kulinda heshima yake.
Simba ambaye msimu huu mambo yamemwendea mrama anatarajia kutumia kikosi kilekile cha makinda wake ambao wanawajenga kwa ajili ya msimu ujao, pia kujiandaa kukumbana na Yanga mechi ya funga pazia ya ligi kuu msimu wa 2012/2013 uwanja wa taifa mwezi mei mwaka huu.
Akiongea na MICHEZO BOMBA! Kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kiwhelu “Julio Alberto” aliseama leo hii mchana wamekaa kikao na wachezaji wao ili kuwapa morali na kuwaeleza umuhimu wa kushinda katika mchezo wa leo.
“Ninavyokuambia hivi tupo katika kikao cha pamoja na wachezaji wetu, tunaelezana machache kabla ya kwenda uwanja wa taifa kuvaana na polisi Morogoro, maandalizi yetu ni mazuri na tuna imani ya kushinda”. Alisema Julio.
Julio aliongeza kuwa mashabiki na wanachama wa wekundu wa smimbazi Simba lazima watambue kuwa timu yao ipo wakati wa mpito, kinachotakiwa kwa wao ni kuwaunga mkono vijana wao ambao wanajengwa kuleta matunda msimu ujao wa ligi.
“Leo hii watu wanaiona Simba haina lolote, sisi tunasema hiki kikosi ambacho kinaandaliwa na benchi la ufundi kitakuwa moto wa kuotea mbali sana, na siku zote tunamshukuru Mungu kwa kutupa uzima na tuna matarajio makubwa sana na vijana wetu”. Alisema Julio.
Wakati Mnyama akijinasibu kushinda mchezo wa leo, nao Polisi Morogoro walisema maandalizi waliyoyafanya yanatosha kupata ushindi mbele ya Simba.
Afisa habari wa klabu hiyo, Clememce Banzo ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa endapo watapoteza mchezo wa leo watazidi kujichimbia kaburi wenyewe na kujizika ndani yake.
“Maji yameshafika shingoni, hakika hatuna hali mpaka sasa na tukifungwa na Simba, safari ya kutoa mkono wa bai bai kwa ligi kuu ya Tanzania bara itakuwa imeshafika”. Alisema Banzo akiwa amekata tamaa.
Banzo aliongeza kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo Rishard Adolf tayari amehawapa mazoezi mazuri na kuwapanga kisaikolojia wachezaji wake kupambana na simba leo hii.
Siku zote soka ni dakika tisini, aliyejipanga na kuwa na nidhamu ya mpira dimbani anaweza kupata ushindi, leo Simba ama Polisi yoyote anaweza kutwaa pointi tatu muhimu, dakika za mwamuzi zinasubiriwa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video