Sunday, April 28, 2013

balozi 
Mshambuliaji nguli wa JKT Ruvu Mussa Hassan Mgunya “Mgosi” (kulia) akifanya vitu vyake katika mechi dhidi ya YangaSONY DSC 
Kikosi cha Keny Mwaisabula “Mzazi”, Wanajeshi wa JKT Ruvu TFF Tanzania Prisons 
Kikosi cha Prisons kinachotaraji kushuka ugani siku ya mei mosi dhidi ya JKT Ruvu

Na Baraka Mpenja
Wakichagizwa na ushindi wa 1-0 dhidi ya Africa Lyon wiki hii, maafande wa jeshi la kujenga taifa JKT Ruvu kutoka mkoani Pwani wapo katika morali kubwa kujiandaa na mchezo wa mei mosi dhidi ya wanajeshi wenzao kutoka jijini Mbeya “Jiji la Kijani”, Wajelajela Tanzania Prisons uwanjwa wa Chamazi Mbande nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo Greyson Haule ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa mpaka sasa wachezaji wote wako salama, hakuna majeruhi yeyote na wana morali kubwa kutokana na kuwepo katika mikono salama ya kusalia ligi kuu Tanzania bara msimu huu.
“Sisi tuko makini sana, wachezaji wangu wote wako barabara, tunarekebisha makosa madogo madogo yaliyoonekana mechi iliyopita, nadhani kufikia siku ya mechi tutakuwa fiti kuwavaa Prisons”. Alisema Haule.
Haule aliongeza kuwa mechi hiyo itakuwa ngumu sana kutokana na timu hizo kuwa sambamba katika msimamo,  wote wakiwa na pointi 26 lakini Prisons wapo juu yao kufuatia wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Prisons yupo nafasi ya 9 wakati Ruvu wapo nafasi ya 10 katika msimamo.
Timu zote mbii zitaweza kusalia ligi kuu bara msimu huu kwani zina pointi nzuri na zinaweza kujichimbia zaidi endapo zitachanga kwa uzuri karata zao za mwishoni.
Wakati huo huo maafande wa Tanzania Prisons leo hii wapo njiani wakisafiri kuja jijini Dar es salaam kwa ajili ya mechi hiyo.
Katibu mkuu wa klabu hiyo Sadick Jumbe alisema wamefanya maandalizi ya kutosha na wameamua kufika siku mbili kabla ya mchezo ili wachezaji wapumzike kabla ya kipute hicho.
“Tuko vizuri, wachezaji wote wapo salama na wana morali kubwa sana kuibuka na ushindi, akina Elias Mguli, Sino Augostino, Henry Mwalugala, Lugano Mwangamba na wengine wengi wote wana morali kubwa kuwaadhibu JKT Ruvu mei mosi”. Alisema Jumbe akiwa njiani.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video