Tuesday, April 30, 2013

1

Na Baraka Mpenja
Homa ya pambano kali la masumbwi ama ndonga la kuwania ubingwa wa IBF Africa baina ya bondia bingwa mtetezi Francis Cheka dhidi ya Thomas Mashali “Simba asiyefugika” inazidi kupanda kwa mashabiki wa wanaume hao wenye ubora zaidi katika mchezo huo.
Rais wa Kampuni ya ngumi za kulipwa Tanzania Yasin Abdallah “Ustadhi” ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa tayari mabondia wote wapo Dar es salaam na leo hii majira ya saa tano asubuhi watapima uzito katika ukumbi wa hoteli ya Nzeka Magomeni Kondoa jijini hapa.
“Hakika tambo zimetawala kila kona huku mashabiki wa mabondia hao wakitambiana kwa hali ya juu, leo hii tunawapima uzito na kesho shughuli yenyewe itaanza ukumbi wa PTA kwa wapinzania hao kupanda ulingoni wakitanguliwa na mapambano ya utangulizi”. Alisema Yasin.
Akizungumzia vipimo vya matumizi ya kuongeza nguvu “Bangi” na mengine mengi, Yasin alisema mabondia wote watapimwa na kama kuna bondia atabainika kutumia madawa hayo yanayokatazwa michezoni  basi atauza ushindi wake kwa mpinzani wake.
Ustadhi aliwaomba mabondia wote watakaocheza mapambano ya utangulizi kujitokeza mapema ili kukamilisha zoezi la upimaji wa uzito kabla ya kuwapima wanaume wawili watakaoshindania gari mpya aina ya Noah.
Kiingilio cha chini katika pambano hilo litakalopambwa na mapambano mengi ya utangulizi kitakuwa shilingi elfu saba za kitanzania (7000/=).
Yasin alisema mashabiki wa mji kasoro bahari Morogoro wamesisitiza kuwa hawatakubali kupoteza ubingwa wao na gari mpya, bali watamuunga mkono Cheka mwanzo mwisho katika ili achukue tena taji hilo.
Kwa upande wa mashabiki wa Mashali wa jijini Dar es salaam wanajigamba kuwa  bingwa wa Afrika Mashariki na Kati “Simba asiyefugika” Thomas Mashali lazima amtandike Cheka ambaye ni mpinzani wake mkubwa kwa sasa.
Tambo zimetawala jijini Dar es salaam huku mashabiki wengi wakimfananisha Cheka na timu za Hispania, Barcelona na Real Madrid kuwa ufalme wake umefika ukingoni na sasa anavua rasmi taji lake.
Kwa upande wa Cheka ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa amezoea maneno ya wapinzani wake, kwani waliwahi kuongea wengi lakini wakaambualia kipigo cha aibu.
“Niko vizuri sana, nimejiandaa kwa umakini mkubwa kutetea ubingwa wangu, mashabiki wangu wa Morogoro wananisapoti sana na sitawangusha hata kidogo”. Alisema Cheka.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video