Sunday, April 21, 2013

soccer-barclays-premier-league-tottenham-hotspur-v-manchester-city-white-hart-lane-9-630x332
UWANJANI White Hart Lane, Tottenham Hospur leo wameitandika Manchester City Bao 3-1 na kujipa matumaini ya kuwemo kwenye 4 Bora ili kucheza ligi ya mabingwa Ulaya Msimu ujao na pia kuwakata maini Man City matumaini yao finyu ya kutetea Taji lao la Ubingwa ambalo kesho Usiku linaweza kuchukuliwa na Mahasimu wao Manchester United ikiwa wataifunga Aston Villa Uwanjani Old Trafford.
City walitangulia kufunga Bao mapema kupitia Samir Nasri katika Dakika ya 5 lakini Bao 3 ndani ya Dakika 6 na Sekunde 20 kuanzia Dakika ya 75 zilizofungwa na Clint Dempsey, Jermain Defoe na Gareth Bale  ziliwasambaratisha Man City.
Tottenham sasa wamefungana Pointi na Chelsea iliyo nafasi ya 4 lakini wanaweza kuishusha Arsenal iliyo nafasi ya 3 ikiwa watashinda Mechi yao moja waliyonayo mkononi.
VIKOSI:
Tottenham: Lloris, Walker, Dawson, Vertonghen, Assou-Ekotto, Sigurdsson, Dembele, Parker, Bale, Dempsey, Adebayor
Akiba: Friedel, Huddlestone, Naughton, Defoe, Holtby, Livermore, Caulker.
Man City: Hart, Zabaleta, Kompany, Nastasic, Clichy, Toure, Barry, Milner, Tevez, Nasri, Dzeko
Akiba: Pantilimon, Lescott, Sinclair, Kolarov, Javi Garcia, Aguero, Kolo Toure.
Refa: Lee Mason

21 Apr 2013

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video