Wednesday, April 24, 2013

One foot in the final: Bayern Munich's Mario Gomez and team mate Javi Martinez celebrate after going 2-0 up

Messi aomba miujiza itokee,katika marejeano
Mabingwa wa mara nne wa michuano ya Ligi ya mabingwa Ulaya,Bayern Munich ya Ujerumani wamejiweka mazingira ya mazuri ya kutinga fainali baada ya kuinyuka Barcelona ya Hispania kwa magoli 4 – 0.
Hiyo ilikuwa nusufainali ya kwanza  ya michuano hiyo maarufu ulimwenguni.
Katika mechi ya  iliyochezwa katika dimba la Allianz Arena ilishuhudia wenyeji wakipata goli la kwanza kupitia kwa Thomas Mueller dakika 25 na Super Mario Gomez dakika ya 49 huku mengine yakiwekwa kimiani na Arjen Robben na Mueller kwa mara nyingine.
Sasa Barcelona watahitaji ushindi wa magoli 5 – 0 katika mechi ya marejeano ili kutinga hatua ya fainali.
Mshambuliaji nyota wa timu hiyo Lionel Messi amesema  timu yake inahitaji miujiza ili kushinda  katika mechi ya marejeano huku akisema ni moja ya kipigo cha aibu kuwakutokea katika kipindi cha ushiriki wao wa ligi ya mabingwa barani Ulaya.
“Magoli 4 – 0 ni pengo kubwa kulifidia katika mechi ya marejeano,itakuwa mechi ngumu kwetu”alisema Messi
Kocha wa Bayern Munich Jupp Heynckes amewaonya wachezaji wake kutojiamini kupita kiasi kwani kuna kibarua cha marejeano chenye dakika 90 zingine kama walizocheza Allianz Arena.
Mshambuliaji Arjen Robben wa Bayern Munich asema “yaani huwezi kuamini ni kama wazimu vile huwezi kuamini tumeshinda magoli 4 – 0 kwa timu iliyotawala Ulaya kwa miaka ya hivi karibuni”

No way back? Messi and Barcelona face an uphill task in the second leg
Barcelona wameruhusu wavu wao kuguswa mara nne katika mechi ya Champions League kwa mara ya kwanza tangu walipofungwa 4-2 na Chelsea katika hatua ya 16 bora Machi 2005.

Kwenye michuano yote ambayo BARCA imeshiriki hivi karibuni haijawahi  kucharazwa kwa magoli  4-0 tangu Getafe ilipowatandika kwa bakora kama hizo katika kombe la mfalme mwaka 2007.
Klabu ya  kwanza kuichapa  Barcelona 4 – 0  katika michuano ya Ulaya ilikuwa ni Dynamo Kiev ya Ukraine  katika hatua ya makundi mnamo  1997.
Kwa historia tu hakuna timu iliyowahi kuchapwa idadi kama hiyo ya mabao katika michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya ikafanikiwa kusonga mbele…….…. Je Barcelona ni mwisho wa enzi?Hapo ni muda utatuambia , vuteni subira mechi ya marejeano Nou Camp nyumbani kwa Barcelona hali itakuwaje? ……..
REAL MADRID,DORTMUND VITANI USIKU WA LEO
Mara baada ya Miamba ya Hispania Barcelona kunyooshwa na wajerumani,Bayern Munich sasa ni zamu ya mahasimu wao Real Madrid kupambana na wajerumani wengine Borussia Dortmund  wakicheza nyumbani  Signal Iduna Park usiku wa leo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video