Friday, April 5, 2013


>>WADAI: ‘HAJUI SHERIA ZA GEMU!!!’
BARCA_HAMASABarcelona wamewasilisha malamiko rasmi kwa UEFA kuhusu uchezeshaji wa Refa Wolfgang Stark walipotoka sare ya Bao 2-2 na Paris St Germain katika Mechi ya kwanza ya Robo Fainali ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGIhivi Juzi.
Barca hawakufurahishwa na uchezeshaji wa Stark na wamedai Refa huyo kutoka Germany ‘hajui Sheria za Gemu’ kwa kuruhusu Mpira uendelee wakati Wachezaji wawili wa Barca, Javier Mascherano na Jordi Alba, walikuwa wamelala chini baada ya kugongana wenyewe.
Barca wamedai Refa huyo alipaswa kusimamisha Mpira wakati huo na pia hakupaswa kulikubali Bao la kwanza la PSG ambalo alifunga Zlatan Ibrahimovic wakati akiwa Ofsaidi.
Msemaji wa Barcelona, Toni Freixa, amesema Klabu yao imewaandikia UEFA kufuatia mlolongo wa makosa ya Refa huyo ikiwa dhahiri kuwa hakufuata Sheria za Soka.
Uamuzi wa kumshitaki Refa huyo UEFA ulichukuliwa na Barcelona baada ya Bodi ya Klabu hiyo kukutana Siku ya Alhamisi.
Msimu huu, Wadau wengi wamekuwa wakilalamika kuhusu uchezeshaji wa Marefa usiokuwa makini hasa baada Mchezaji wa Manchester United, Nani, kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu Man United walipofungwa 2-1 na Real Madrid lakini tukio kama la Nani lilifanywa mara mbili na Wachezaji wa Real Madrid walipoifunga Galatasaray Bao 3-0 juzi Jumanne lakini Wachezaji wa Real hawakupewa Kadi yeyote.

KUTOKA SOKA IN BONGO

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video