Tuesday, March 12, 2013

>>BARCA KUPINDUA KICHAPO 2-0 CHA AC MILAN??
>>TAYARI ROBO FAINALI: REAL, DORTMUND, JUVE & PSG!
>>NANI KUUNGANA NAO??
JUMANNE na JUMATANO Usiku zipo Mechi 4 za Marudiano za Raundi ya Mtoano ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, lakini kwa Jumanne, macho, masikio na kila kitu kitakuwa huko Nou Camp kushuhudia kama ile inayodaiwa Timu Bora Duniani, FC Barcelona, itaweza kupindua kipigo cha Bao 2-0 na kuibwaga nje AC Milan.
+++++++++++++++++++++++++++
RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16
RATIBA:
-Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne 12 Machi 2013
Barcelona v AC Milan [0-2]
Schalke v Galatasaray [1-1]
Jumatano 13 Machi 2013
Bayern Munich v Arsenal [3-1]
Malaga v FC Porto [0-1]
+++++++++++++++++++++++++++
BARCA_v_AC_MILAN_SQUADSAC Milan, inayoongozwa na Kocha Massimiliano Allegri, inatumbukia Nou Camp kuivaa Barcelona baada ya kuifunga Bao 2-0 katika Mechi yao ya kwanza kwa Bao za Kevin-Prince Boateng na Sulley Muntari Uwanjani San Siro.
Barca, baada ya kufungwa na AC Milan, ilipata pigo kubwa ilipofungwa mara mbili mfululizo ndani ya Wiki moja na Mahasimu wao wakubwa Real Madrid, kwanza kwa Bao 3-1 na kubwagwa nje ya Copa del Rey na kisha 2-1 kwenye La Liga, lakini juzi Jumamosi iliifunga Deportivo La Coruna Bao 2-0 kwenye La Liga.
Nao AC Milan, majuzi Ijumaa, walliwachapa Genoa Bao 2-0 kwenye Mechi ya Serie A lakini walipata pigo kubwa pale Straika wao wa kutegemewa, Giampaolo Pazzini, alipovunjika mfupa wa mguu na pia hawawezi kumchezesha Straika wao mwingine Mario Balotelli ambae ameshacheza Mashindano haya Msimu huu akiwa na Manchester City.
+++++++++++++++++++++++++++
DONDOO MUHIMU:
-KLABU hizi zimekutana mara 16, Barca wakishinda mara 6 na AC Milan mara 5 huku Barca wakipiga Bao 22 na AC Milan 21.
-NOU CAMP: Barca Wameshinda Mechi 3 Sare 3 na AC Milan Wameshinda 1
-MSIMU uliopita walikutana Robo Fainali ya UCL wakatoka 0-0 huko San Siro na Barca kushinda 3-1 Nou Camp kwa Bao 2 za Penati za Lionel Messi na moja la Iniesta huku Bao la AC Milan kufungwa na Antonio Nocerino.
-MSIMU WA 2011/12 walikuwa Kundi moja na Mechi ya kwanza Nou Camp ilikuwa 2-2 na huko San Siro Barca walishinda 3-2
+++++++++++++++++++++++++++
Kocha wa muda wa Barcelona, Jordi Roura, ambae anashikilia wadhifa huo kwa vile Kocha Mkuu Tito Vilanova yuko kwenye matibabu ya ugonjwa wa Kansa, ametoa onyo kuwa Wachezaji wake wako tayari kwa changamoto hii ya AC Milan.
Ametamka: “Tunajua wazi jinsi tutakavyocheza na Milan na wao wanataka sisi tucheze vipi.”
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
BARCELONA: Victor Valdes, Dani Alves, Gerard Pique, Carles Puyol, Adriano, Sergio Busquets, Xavi, Andres Iniesta, David Villa, Lionel Messi, Pedro
AC MILAN: Christian Abbiati, Ignazio Abate, Philippe Mexes, Cristian Zapata, Kevin Constant, Massimo Ambrosini, Sulley Muntari, Riccardo Montolivo, Kevin-Prince Boateng, Stephan El Shaarawy, M'Baye Niang
SCHALKE v GALATASARAY
Timu hizi zilitoka sare ya Bao 1-1 huko Telekom Arena, Nchini Uturuki na Jumanne wanarudiana Uwanjani Vetins Arena Nchini Ujerumani na Schalke wako imara sana baada ya kushinda Mechi zao zote tangu sare hiyo ikiwemo ushindi wa Bao 2-1 dhidi ya Mabingwa wa Germany Borussia Dortmund juzi Jumamosi kwenye Mechi ya Bundesliga.
UCL: RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16
RATIBA:
-Mechi kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumatano 13 Machi 2013
Bayern Munich v Arsenal [3-1]
Malaga v FC Porto [0-1]
+++++++++++++++++++++++++++

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video