Wednesday, March 6, 2013


UEFA_CHAMPIONZ_LIGI_LOGO-BOMBAZ>>NANI KUTINGA ROBO FAINALI??
MECHI za Marudiano za UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, zinaendelea leo kwa Mechi mbili kati ya Juventus na Celtic huku Juve wakiongoza kwa Bao 3-0 toka Mechi ya Kwanzawaliyoshinda ugenini na Paris St Germain kurudiana na Valencia waliyoifunga Bao 2-1 ugenini.
+++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
-Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku
-Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza
Jumatano 6 Machi 2013
Juventus v Celtic [3-0]
Paris St Germain v Valencia [2-1]
+++++++++++++++++++++++++++++
DONDOO MUHIMU:
PARIS SAINT-GERMAIN FC V VALENCIA CF (2-1)
PSG wamewahi kushinda Mechi zao zote 13 za Mashindano ya UEFA baada ya kupata ushindi wa ugenini katika Mechi ya kwanza lakini hii ni mara ya kwanza kwao kutinga Raundi ya Mtoano tangu Mwaka 1994/95 ambako walikomea Nusu Fainali.
Kipigo cha Valencia cha 2-1 mikononi mwa PSG katika Mechi ya kwanza kimevunja ile Rekodi ya Valencia ya kutofungwa na Klabu za France katika Mechi 17.
Hata hivyo, Valencia hadi sasa hawajafungwa na Klabu yeyote ya France katika Mechi 8 walizocheza Nchini France ambazo wameshinda 4 na sare 4.
JUVENTUS V CELTIC FC (3-0)
Juventus hawajafungwa kwenye Mashindano ya Klabu Barani Ulaya tangu Tarehe 18 Machi 2010 walipochapwa Bao 4-1 Uwanjani Craven Cottage na Fulham kwenye UEAF EUROPA LIGI na ubwagwa nje kwa Jumla ya Bao 5-4 kwa Mechi mbili.
Baada ya hapo, Juventus, katika Mechi za Ulaya, wameshinda Mechi 8 na sare 9 huku wakishinda Mechi zao 4 zilizopita bila kufungwa hata Bao moja.
Celtic, wakicheza Raundi hii kwa mara ya kwanza katika Misimu mitano, hawajawahi kushinda hata mara moja katika Mechi zao 9 walizocheza Italy.
Katika Mechi zao 20 na Klabu za Italy Matokeo ni Ushindi 5, Sare 7 na Kufungwa 8 huku zile zilizochezwa Nchini Italy zikiwa Ushindi 0, Sare 3 na Kufungwa 9.
Kumbukumbu kubwa ya Celtic ni ya yale Mashindano yao ya kwanza Barani Ulaya ambapo walifanikiwa kuwa Klabu ya kwanza toka Uingereza kutwaa Kombe la Ulaya kwa kuichapa Inter Milan Bao 2-1 kwenye Fainali huko Lisbon, Ureno Mwaka 1966/67.
UCL: RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16
RATIBA:
-Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku
-Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza
Jumanne 12 Machi 2013
Barcelona v AC Milan
Schalke v Galatasaray
Jumatano 13 Machi 2013
Bayern Munich v Arsenal
Malaga v FC Porto
+++++++++++++++++++++++++++
ROBO FAINALI:
Mechi ya 1=Tarehe 2 na 3 Aprili 2013
Mechi ya 2= Tarehe 9 na 10 Aprili 2013
NUSU FAINALI
Mechi ya 1= Tarehe 23 na 24 Aprili 2013
Mechi ya 2= Tarehe 30 Aprili  na 1 Mei 2013
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, London.
kutoka soka in Bongo Leo

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video