Laurent Koscielny akifunga bao la pili kwa kichwa dakika za mwishoni |
Kipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer akiuzuia mpira dhidi ya wachezaji wa Arsenal baada ya kufungwa bao la pili, ili kupoteza muda |
Olivier Giroud akifunga bao la mapema lililowatia presha wenyeji |
>>ROBO FAINALI KAMILI: REAL, DORTMUND, JUVE, PSG, BARCA, GALATASARAY, BAYERN & MALAGA!
>>DROO NI IJUMAA!!!
>>NI MARA YA KWANZA TANGU 1995/6 ENGLAND KUTOKUWA NA TIMU ROBO FAINALI!!
ARSENAL
leo walikufa kiume huko Allianz Arena Jijini Munich kwa kuitwanga
Bayern Munich Bao 2-0 na kufanya Mechi mbili kati yao kuwa Jumla Bao 3-3
lakini wamekwenda nje ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, kwa Mabao ya ugenini
kwa vile wao walipigwa kwao Emirates Bao 3-1 na kuiacha Bayern
ikitiririka Robo Fainali.
Safu ya Robo Fainali ya Timu 8
imekamilika kwa Malaga nao kushinda Bao 2-0 dhidi ya FC Porto ambao
waliifunga Malaga Bao 1-0 katika Mechi ya Kwanza.
Droo ya kupanga Mechi za Robo Fainali itafanyika Ijumaa Machi 15.
MALAGA 2 FC PORTO 0
Malaga, wakicheza kwao huku wakiwa nyuma
kwa Bao 1-0 toka Mechi ya kwanza, wamefanikiwa kuingia Robo Fainali
baada ya kuipiga FC Porto Bao 2-0.
+++++++++++++++++++++++++++
MAGOLI:
Malaga 2
-Isco Dakika ya 43
-Santa Cruz 77
FC Porto 0
+++++++++++++++++++++++++++
FC Porto walicheza Mechi hii tangu Dakika ya 49 wakiwa Mtu 10 pale Defour alipopewa Kadi Nyekundu.
VIKOSI:
Malaga: Willy, Jesus Gamez, Demichelis, Weligton, Antunes, Joaquin, Toulalan, Iturra, Isco, Julio Baptista, Saviola
Akiba: Kameni, Lugano, Camacho, Fernandez, Piazon, Sergio Sanchez, Santa Cruz.
FC Porto: Helton, Danilo, Otamendi, Mangala, Alex Sandro, Joao Moutinho, Fernando, Gonzalez, Varela, Martinez, Defour
Akiba: Fabiano, Maicon, Andre Castro, Rodriguez, Izmailov, Liedson, Atsu.
Refa: Nicola Rizzoli (Italy)
BAYERN MUNICH 0 ARSENAL 2
Arsenal walianza Mechi hii vizuri sana
kwa kupata Bao la mapema katika Dakika ya 3 tu kupitia Giroud kufuatia
kazi njema ya Theo Walcott.
+++++++++++++++++++++++++++
MAGOLI:
Bayern 0
Arsenal 2
-Giroud Dakika ya 3
-Koscielny 86
+++++++++++++++++++++++++++
Ili kutinga Robo Fainali, Arsenal
walitakiwa wapiga Bao 3 lakini walimudu Bao mbili tu baada ya Koscielny
kuipatia Bao la pili kwa kichwa katika Dakika ya 86.
Ushindi huu wa Arsenal wa Bao 2-0
haukutosha kwa kuwa walipigwa kwao Bao 3-1 na Jumla ya Magoli kwa Mechi
mbili ni 3-3 na Bayern kupenya kwa wingi wa Magoli ya ugenini.
VIKOSI:
Bayern Munich: Neuer; Lahm, Dante, Van Buyten, Alaba; Martinez, Gustavo; Muller, Kroos, Robben; Mandzukic
Akiba: Starke, Rafinha, Contento, Shaqiri, Tymoshchuk, Pizarro, Gomez.
Arsenal: Fabianski; Jenkinson, Mertesacker, Koscielny, Gibbs; Arteta, Ramsey; Walcott, Rosicky, Cazorla; Giroud
Akiba: Mannone, Arshavin, Vermaelen, Ox, Diaby, Gervinho, Coquelin.
Refa: Pavel Kralovec (Czech Republic).
+++++++++++++++++++++++++++
ROBO FAINALI:
Mechi ya 1=Tarehe 2 na 3 Aprili 2013
Mechi ya 2= Tarehe 9 na 10 Aprili 2013
NUSU FAINALI
Mechi ya 1= Tarehe 23 na 24 Aprili 2013
Mechi ya 2= Tarehe 30 Aprili na 1 Mei 2013
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, London.
0 comments:
Post a Comment