>>RON ATKINSON: ‘GIGGS ANAKUFANYA UAMINI KUNA MUNGU WA SOKA! ‘
>>GEORGE BEST: ‘IPO SIKU WATU WATASEMA MIE NILIKUWA GIGGS MWINGINE!!’

Aliemgundua Ryan Giggs ni Wakala wa
Magazeti na ambae pia alikuwa Mlinzi wa Old Trafford, Harold Wood,
aliemdokeza Alex Ferguson kuhusu Chipukizi huyo na Ferguson akatuma Mtu
kwenda kuchunguza na hatimae Giggs akapewa Majaribio na Man United
Krismas ya Mwaka 1986.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
GIGGS NDIE MWENYE REKODI UINGEREZA KWA MATAJI MENGI:
-UBINGWA LIGI KUU: 12
-FA CUP: 4
-LIGI CUP: 3
-CHAMPIONZ LIGI: 2
-NA MENGINE MENGI!!!
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
SIR ALEX FERGUSON:
-Nakumbuka mara ya kwanza
kumuona, alikuwa na miaka 13 na alikuwa akielea kama ndege mdogo angani
anaekimbiza karatasi kwenye upepo!
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Baada ya hapo, Giggs, akiwa na Miaka 13
tu, aliongoza Timu yake Salford Boys kucheza na Kikosi cha Vijana wa
chini ya Miaka 15 cha Man United na alipiga hetitriki huku Ferguson
akiwa kwenye Dirisha la Ofisi yake akishuhudia.
Alipotimiza Miaka 14, Tarehe 29 Novemba
1987, Sir Alex Ferguson, alikwenda Nyumbani kwa kina Giggs na kumpa Ofa
ya kusainiwa kwa Miaka miwili kama Mchezaji Chipukizi Mwandamizi toka
Shuleni.
HAPO NDIO HISTORIA INAYOENDELEA ILIPOANZA…………………..
NINI WANASEMA JUU YAKE:
-MARTIN KEOWN: Nilipomwona mara ya kwanza akicheza alikuwa Mtoto, mwembamba sana …sasa Lejendari!!
-ALESSANDRO DEL PIERRO: Ni Wachezaji wawili tu hunifanya nilie nikiwaona wakicheza, mmoja ni Diego Maradona na mwingine Ryan Giggs!!
-JOHAN CRUYFF: Eric Cantona ni Mchezaji Bora lakini hamfikii Ryan Giggs!!
-BRIAN KIDD: Kipaji chake amepewa na Mungu. Atabakia na Kipaji hicho hicho hata kama atastaafu kwa sababu kipaji aina hii hakitoweki!!
-RON ATKINSON: Giggs anakufanya uamini kuna Mungu wa Soka!
-GEORGE BEST: Ipo Siku Watu watasema mie nilikuwa Giggs mwingine!!
-PAUL SCHOLES: Wapo Wachezaji Bora sana nimecheza nao Timu moja lakini kama kuchagua Bora ni Giggs, anaweza kufanya chochote!!
-FERGUSON: Ryan anaweza kuwafanya Mabeki Damu zao zipinde!!
imehamishika kutoka blog ya soka in bongo
0 comments:
Post a Comment