Saturday, March 9, 2013


Jumamosi, 09 Machi 2013 09:35
Chapisha Toleo la kuchapisha
MANDZUKICSTRAIKA wa Bayern Munich Mario Mandzukic amesema wao nia yao ni ‘kupasha moto’ kwa kuifunga Fortuna Duesseldorf leo kwenye Bundesliga yakiwa ni matayarisho yao kwa ujio wa Arsenal hapo Jumatano Uwanjani Allianz Arena ikiwa ni Mechi ya Marudiano ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI huku Bayern wakiwa kifua mbele baada ya kuifumua Arsenal Bao 3-1 katika Mechi ya kwanza iliyochezwa Emirates Wiki mbili zilizopita.
+++++++++++++++++++++++++++
BUNDESLIGA
Ijumaa Machi 8
FC Augsburg 1 FC Nuremberg 2
Jumamosi Machi 9
Bayern Munich v Fortuna Dusseldorf
Schalke 04 v BV Borussia Dortmund
SC Freiburg v VfL Wolfsburg
FSV Mainz 05 v Bayer 04 Leverkusen
SpVgg Greuther Furth v TSG Hoffenheim
Borussia Mönchengladbach SV v Werder Bremen
Jumapili Machi 10
Hannover 96 v Eintracht Frankfurt
VfB Stuttgart v Hamburger SV
+++++++++++++++++++++++++++
Kwenye Bundesliga, huku Mechi zikiwa zimebaki 10, Bayern Munich wako kileleni wakiwa Pointi 17 mbele ya Timu ya Pili, Mabingwa watetezi Borussia Dortmund.
+++++++++++++++++++++++++++
MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 24]
Bayern Munich Pointi 63
BV Borussia Dortmund 46
Bayer 04 Leverkusen 45
Eintracht Frankfurt 38
SC Freiburg 36
Schalke 04 36
Hamburger SV 35
FSV Mainz 05 34
Borussia Mönchengladbach 34
+++++++++++++++++++++++++++
Mara ya mwisho kwa Fortuna Dusseldorf kuifunga Bayern ilikuwa ni Aprili 1991 na Mechi zote 3 zilizofuata Bayern walishinda bila kufungwa hata Goli moja.
Hata hivyo, Mandzukic amesema wanaiheshimu Fortuna lakini wao wako tayari kuikabili.
Aliongeza: “Tuko nyumbani na tunataka kuongeza wimbi letu la ushindi. Wengi wanafikiri tushaingia Robo Fainali ya UCL lakini lolote linaweza kutokea kwenye Soka.”
Mandzukic alifunga Bao la 3 wakati Bayern ilipoipiga Arsenal 3-1 na Bao nyingine zao kufungwa na Kroos na Muller wakati la Arsenal lilifungwa na Podolski.
Wakiwa tayari wametinga Robo Fainali ya UCL baada ya kuifunga Shakhtar Donetsk, Mabingwa Borussia Dortmund wanasafiri Kilomita 40 kucheza na Jirani zao Schalke 04 ambao wameshinda Mechi moja tu kati ya 5 za Bundesliga walizocheza na Dortmund na hiyo ya ushindi ni Bao 2-1 walioupata nyumbani kwa Dortmund Uwanja wa Signal Iduna Park Mwezi Oktoba Mwaka jana.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video