>>ALIJIUZULU MARA BAADA YA NIGERIA KUTWAA UBINGWA AFRIKA!!
>>KESHI & EL GOHARY NDIO PEKEE MABINGWA AFRIKA KAMA WACHEZAJI NA MAKOCHA!
Stephen
Keshi atabakia kama Kocha wa Mabingwa wapya wa Afrika, Nigeria,
kufuatia kuingilia kati kwa Waziri wa Michezo wa Nchi hiyo, Bolaji
Abdillahi, aliemshawishi afute msimamo wake wa kujiuzulu alioutoa mara
baada ya kufanikisha Nchi yake kutwaa Ubingwa wa AFCON 2013 Jumapili
huko Afrika Kusini kufuatia mgogoro wake na Shirikisho la Soka, NFF.
Jumatatu, Keshi alitangaza kujiuzulu wakati akiongea kwenye Kituo cha Redio cha Afrika Kusini, Metro FM.
Lakini Waziri wa Michezo wa Nigeria ,
ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Kitaifa ya Michezo ya Nigeria,
aliingilia kati na kumshawishi Keshi, mwenye Miaka 51, afute uamuzi huo
walipokutana Jumatatu huko Johannesburg, Afrika Kusini.
Keshi aliafikiana na Waziri wa Michezo, Bolaji Abdillahi, na sasa ataendelea kuwa Kocha wa Nigeria.
Pia, imebainishwa kuwa Kikao cha kusaka
muafaka kati ya Keshi na NFF kitafanyika huko Abuja mara baada ya
Mabingwa hao kutua huko Abuja ambako watapokelewa kwa shangwe na
Wanigeria na kukaribishwa Ikulu kukutana na Rais wa Nigeria.
Jumapili iliyopita, kwenye Uwanja wa
FNB, Soccer City, Soweto, Johannesburg, Nigeria walitwaa Kombe la
Ubingwa wa Afrika walipoichapa Burkina Faso Bao 1-0 na hii ni mara yao
ya 3 kuwa Mabingwa baada ya kushinda Mwaka 1980 na 1994.
Stephen Keshi ni Mtu pekee, baada ya
Mahmoud El Gohary wa Egypt, kuweza kutwaa Ubingwa wa Afrika kama
Mchezaji na Kocha wa Nchi yake.
SOKA IN BONGO
0 comments:
Post a Comment