Friday, January 18, 2013



DARREN_FLETCHERKiungo wa Manchester United Darren Fletcher ataukosa Msimu huu uliobakia baada ya kwenda kufanyiwa Operesheni ili kutibu ugonjwa sugu wa Tumbo uliokuwa ukimsibu kwa muda mrefu na kumfanya awe nje ya Uwanja kwa Miezi 11 kuanzia Desemba 2011 na kurejea tena mwanzoni mwa Msimu huu.
Msimu huu alicheza Jumla ya Mechi 13 kwa Manchester United na Nchi yake Scotland na Mechi yake ya mwisho ilikuwa ni kuingizwa kutokea Benchi katika Dakika ya 89 Manchester United walipoifunga Newcastle 4-3 hapo Desemba 26, 2012.
++++++++++++++++++++++++
WASIFU wa FLETCHER:
-UMRI: 28
-MECHI MAN UNITED: 310 MAGOLI: 23
-MECHI SCOTLAND: 61 MAGOLI: 7
-MATAJI: 4 UBINGWA LIGI KUU (2007, 2008, 2009, 2011), 1 FA CUP (2004), 2 LIGI CUP (2006, 2010), 1 CHAMPIONS LEAGUE (2008), 1 WORLD CLUB CUP (2008)
-MECHI ya KWANZA: Man United v BASEL, 12 Machi 2003 (UEFA Champions League)
-MECHI ya MWISHO: Man United v NEWCASTLE, 26 Desemba 2012 (Barclays Premier League)
++++++++++++++++++++++++
Klabu ya Manchester United imethibitisha habari hizi na kusema Opersheni hiyo ilikuwa imepangwa.
Akizungumzia habari hizi, Meneja mpya wa Scotland, Gordon Strachan, amemtakia kila heri Darren Fletcher, ambae ni Nahodha wa Timu ya Taifa ya Scotland, na pia kusisitiza Fletcher atabaki kama Nahodha na yupo kwenye mipango yake ya baadae.
Fletcher anao Mkataba na Manchester United hadi Mwaka 2011.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video